Kuhusu milion 50 Za mh. Magufuli

Wakati Rais John Pombe Magufuli akiwania nafasi ya kuiongoza Tanzania aliahidi kutoa shilingi Milioni hamsini kwa kila kijiji .
Leo Mei 10 2016 hoja imeingizwa Bungeni na Mbunge wa viti maalum Esther Mahawe ameuliza Swali…>>’ Je, ni lini fedha hizo zitatolewa? Pili Serikali imejipanga vipi kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi juu ya njia bora ya kutumia fedha hizo? ‘
Nakukutanisha na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Abdallah Possi …>>>’ Serikali imetenga shilingi bilioni 59.5 katika bajeti ya mwaka 2016/2017 chini ya fungu 21 kwa ajili ya kuwezesha wananchi vijijini kwa kutoa shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na mtaa‘
‘ Fedha hizo zitatolewa baada ya kuidhinishwa na Bunge na baada ya kukamilisha taratibu zinazolenga kuhakikisha uwepo wa tija katika matumizi ya fedha hizo ‘
‘ Ili kuhakikisha matumizi bora ya fedha hizo Serikali imeendelea kukamilisha maandalizi ya utaratibu maalum wa utoaji fedha hizo ikiwa ni pamoja na utoaji wa elimu ya ujasiriamali‘

Comments

Popular posts from this blog

NEW VIDEO: Korede Bello - Do like that