VIDEO: Majibu ya Linex kuhusu kuhamia kwenye muziki wa injili
Baada ya headline kuandikwa kwamba hivi sasa staa wa bongoflava Linex Sunday Mjeda ameamua kuachana na style ya muziki wake na kuhamika kwenye muziki wa injili, Linexmwenyewe amesimama mbele ya camera ya. SHAYO TV nakusema kuwa bado hajafikilia kuhamia moja kwa moja ingawa anatarajia kuachia midundo ya injili.
‘Mungu anatutoa mbali sana watu, hata ukiwa wa shetani inapaswa urudishe moyo wako na umsifu Mungu baba, nilipotoka na hapa nilipo wacha nimshukuru yeye‘ –Linex
‘Mwaka huu nitarekodi muziki wangu wa kawaida lakini nitarekodi na nyimbo za injili na hadi sasa ninazo ngoma mbili kwahiyo sifikiri kama ni kitu kibaya kufanya hata muziki wa injili kwa lengo la kumshukuru Mungu‘ –Linex
Tazama video hapa chini
Comments